ENG    SWA   FR

Salamu Za Aprili 2025

Blinky Bill(Kenya)

AHSANTE!

Shukrani za dhati kwa kila mmoja aliyeshiriki nasi kwa tamasha la 22 la Sauti za Busara 2025, Bila ninyi tusingefanikiwa! kwapamoja, tulicheza, tulimba, tulisherehekea, na tulitengeneza kumbukumbu nzuri  hadi mwisho wa tamasha.

Upendo wenu, na shauku yenu zilifanya toleo la 22 kuwa lenye mafanikio makubwa, na tunashukuru sana kuwa nanyi kama sehemu ya familia yetu. Tunapomaliza tamasha la mwaka huu, tunasema ASANTE SANA kutoka kwenye mioyo yetu. Kauli mbiu “Voices for peace” iliguswa sana kupitia tamasha hili, na tunatumai itabaki katika nyoyo zetu daima, ikitufundisha kueneza ujumbe wake popote tutakapokwenda. Amani itufungue kwenye kila tunalofanya, mpaka tutakapokutana tena. 

Tunakusubiri tena kufanya yote haya mwaka kesho, Yajayo ni mazuri zaidi!

 Tutaonana 2026!

 

Ili kupata ladha kidogo ya kile kilichojiri katika tamasha Sauti za Busara 2025 tafadhali tazama viungo vilivyo hapa chini!

Media Coverage
View the impression video/Matukio yaliyojiri
Busara Website
ASSA-MATUSSE-Mozambique
Call for Artists 2025
Wito Kwa Msanii

Wito kwa Wasanii sasa umefunguliwa kwa Toleo la 23 la tamasha la Sauti za Busara, kama ilivyopangwa kutikisa kuta za Mji Mkongwe, Zanzibar wakati wa 06 - 08 Februari 2026.

Sauti za Busara huonyesha muziki wa aina mbalimbali kutoka Bara la Afrika na ughaibuni. Wanamuziki wanaowakilisha Ulimwengu wa Kiarabu na eneo la Bahari ya Hindi pia wanakaribishwa kutuma maombi.

Wito kwa Wasanii umefunguliwa hadi tarehe 31 Julai 2025 pekee.

Upendeleo hutolewa kwa:

  • Muziki asilia wenye utambulisho wa kitamaduni ambao umeunganishwa na Afrika.
  • Wasanii wanawake, au vikundi vinavyoongozwa na wanawake
  • Vijana, vipaji vipya na vinavyochipukia
  • Muziki wenye ujumbe chanya, muhimu, na muhimu kwa jamii
  • Muziki unaoimbwa ‘100% live’!!

 

Kwa taarifa zaidi juu ya Wito kwa wasanii na Fomu ya Maombi Fungua kiunga hapa chini!

Sauti za Busara 2024 audience
Sauti za Busara Partners & Supporters

Shukrani za Pekee kwa Wadhamini na Wafadhili wetu!

Tangu mwaka 2004, Sauti za Busara imekuwa ikileta watu kutoka kila kona ya dunia kuja Zanzibar. Kila mwaka mwezi wa Februari, tunakusanyika pamoja kusherehekea utajiri na utofauti wa muziki wetu na urithi wetu wa kitamaduni.

Hii ingekuwa ni vigumu bila kuwa na wadau, ambao tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati. Shukrani maalum kwa Fumba Town, mdhamini wetu mkuu wa NGO inayosimamia Tamasha hili, pamoja na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Clouds Media, Umoja wa Ulaya, UN Women, Kenya Airways, na wadhamini wetu wote kwa Toleo la 22 la Sauti za Busara.

Tafadhali tembelea tovuti zao na mitandao yao ya kijamii na tumia huduma na bidhaa zao bora!

Tunatarajia kukuona tena mwaka 2026!

Wako, Timu  Busara

 

Fumba Town
Clouds Media Logo
Kenya Airways Logo
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
EU
UN WOMEN
Zanlink Logo (without LT) CMYK copy-1.png
Volks House
Embassy of France
Airtel
infinity-Logo
Little Gig
Zanzibar-Insurance-Company
Cape-Town-Fish-Market
FTS
Spice Island Interiors
Sauti za Busara - One Africa

Follow us on Social Media to get the latest updates:

This e-mail has been sent to [[EMAIL_TO]], click here to unsubscribe.

Busara Promotions. Maisara, Stone Town 3635 Zanzibar City TZ