Orodha ya Wasanii Kutangazwa Oktoba 2025

Sauti za Busara Line-Up 2026

Kutangazwa kwa Orodha ya Wasanii Oktoba 2025!

Jiandae kwa toleo la 23 la Sauti za Busara litakalowasha moto mitaa ya Stone Town, Zanzibar kuanzia tarehe 5 hadi 8 Februari 2026! Mwaka huu, tunafuraha kutangaza orodha ya wasanii mahiri, wakiongozwa na gwiji wa muziki wa Afrika.

Kwa mara ya kwanza kabisa, Salif Keita, anayejulikana kama “The golden voice of  Afrika,” atapanda jukwaani katika tamasha la Sauti za Busara. Onyesho lake litaweka historia si tu kwa tamasha hili bali pia kwa muziki wa Afrika, likiwaunganisha vizazi kupitia sauti, roho, na simulizi. Kutoka moyo wa Mali hadi pwani za Zanzibar, ujio wa Salif Keita unasherehekea nguvu ya urithi wa Kiafrika na roho ya mshikamano inayobeba maana ya Sauti za Busara.

Ataungana na wasanii wengine mahiri na chipukizi kutoka kila pembe ya bara la Afrika na mataifa ya diaspora. Ben Pol (Tanzania), Man Fongo (Tanzania), Pilani Bubu (South Africa), Lindigo (Réunion), Malcolm Jiyane Tree-O (South Africa), Sousou & Maher Cissoko (Senegal & Sweden), Kara Sylla & Baye Fall Band (Switzerland), Hammer Q (Zanzibar), Atanda & Afrojazz Messengers (Nigeria & UK), Tarajazz (Zanzibar), La Carmen Y Su Familia Musical (Colombia), Mehmet Polat Quartet (Netherlands) .

Orodha ya wasanii wengine ni kama  Alamokha (Tanzania), Mama C & The Fusion Band (Tanzania), Magomamoto Theatre Group (Tanzania), Man Kifimbo (Tanzania), Labdi (Kenya), Ancestors (Togo), Abdel Grooz (Canada & Algeria), Bilal Irshed Trio (Ghana, Palestine & Denmark), Ahamada Smis (Comoros), Seby Ntege (Uganda), Kaya Byinshii (Rwanda), Rajab Suleiman & Kithara (Zanzibar), DCMA Young Stars (Zanzibar) Swahili Encounters (Various),na wengine wengi!

Tazama orodha nzima!
Early Bird Ticket  2025

Nunua Tiketi Sasa!

Usikose nafasi yako ya kuhudhuria toleo lijalo la Sauti za Busara! Tiketi za Mapema(Early Bird) sasa zinapatikana kununuliwa mtandaoni kupitia jukwaa la Tukiio, tovuti rasmi ya Sauti za Busara, na ofisi za Busara Promotions.

Chukua tiketi yako leo upate bei nafuu na ufurahie uzuri wa Sauti za Busara mwaka 2026!

VIP Tickets za Awali kwa wakazi wa ndani na wageni wa kimataifa tayari zimeuzwa zote! Usikose nafasi yako—tiketi za kawaida bado zinapatikana, lakini mauzo yanafungwa tarehe 31 Oktoba 2025. Hii ndiyo nafasi yako ya kuwa sehemu ya tukio kubwa zaidi la muziki Afrika Mashariki!

Kwa bei za tiketi pamoja na masharti na vigezo, tembelea tovuti yetu.

Nunua tiketi hapa!
Dogo Fara (Réunion) at Sauti za Busara 2024
Sholo Mwamba (Tanzania) at Sauti za Busara 2024
Mádé Kuti & The Movement (Nigeria)
Stone Town, Zanzibar

Maelezo kwa wageni!

Ili kupanga safari yako kuja Zanzibar, tembelea ukurasa wa wageni kwenye tovuti yetu. Sehemu hii inatoa taarifa muhimu kuhusu  hoteli, visa, mahitaji ya kiafya, chanjo, na mengine mengi!

Karibu Zanzibar! 
Call for Media Accreditation 2025

Wito Kwa Waandishi wa habari!

Sauti za Busara 2026 inatua Mji Mkongwe, Zanzibar kuanzia tarehe 5 hadi 8 Februari, kwa siku nne za burudani ya moja kwa moja ya muziki wa Kiafrika katika eneo la Urithi wa Dunia la UNESCO. Mwaka huu, orodha ya wasanii ikiongozwa na Salif Keita Sthe golden voice of Africa, atakayetumbuiza kwa mara ya kwanza kwenye tamasha hili.

Wataalamu wa vyombo vya habari sasa wanaweza kuomba idhini maalum za waandishi wa habari, wapiga picha, na waandaaji wa filamu, kwa nafasi kuripoti kuhusu wasanii mashuhuri wa Afrika katika tamasha hatua itakayoongeza thamani kwenye wasifu wako wa kazi na kukuza hadhi yako kimataifa.

Usajili wa mapema ni wa lazima, na kipaumbele kitatolewa kwa wale waliowahi kuunga mkono tamasha hili hapo awali.

Usajili uko wazi hadi tarehe 31 Desemba 2025.

Jiandikishe hapa !
2025 Call for Movers & Shakers

Usajili wa Movers & Shakers

Sauti za Busara huwakusanya wapenda muziki na wataalamu wa tasnia kutoka duniani kote, na kiini cha tamasha hili ni jukwaa letu la siku mbili la sekta ya muziki, Movers & Shakers.

Hili ni eneo linalowaunganisha wasanii wa ndani na wa kimataifa, wasimamizi, mapromota, vyombo vya habari, na viongozi wa kitamaduni kwa ajili ya kuunganishwa, kushirikiana, na kubadilishana mawazo yanayounda mustakabali wa muziki wa Kiafrika.

Iwapo unatafuta kupanua mtandao wako, kuanzisha ushirikiano mpya, kupata nafasi za kutumbuiza, au kujifunza kutoka kwa sauti za sekta ya muziki duniani, Movers & Shakers ndilo jukwaa sahihi kwako.

Hili si tu mazungumzo, ni mwanzo wa fursa mpya katika kazi yako

Kuingia ni bure, na nafasi ni chache. Jisajili sasa uhakikishe nafasi yako ya kuwa sehemu ya majadiliano yenye umuhimu.

Usajili uko wazi hadi tarehe 31 Januari 2026.

Jisajili hapa Movers & Shakers 2026
Sauti za Busara 2024 Highlight Video

Sauti za Busara inajivunia kushirikiana na UNESCO na WOMEX katika ushirikiano wenye nguvu unaolenga kuendeleza utofauti wa tamaduni, usawa wa kijinsia na maendeleo endelevu kupitia muziki. Kupitia msaada wa UNESCO na mtandao wa kimataifa wa WOMEX, ushirikiano huu unaimarisha mafunzo kwa wasanii na mameneja, kukuza maendeleo yao kitaaluma, na kuwapa jukwaa la kimataifa kuhakikisha kuwa urithi wa muziki wa Afrika unaendelea kudumu kwa vizazi vijavyo.

Tazama Video Hapa
Womenx 2024

WOMEX 2025

 WOMEX 25 itafanyika mjini Tampere, Finland kuanzia tarehe 22 hadi 26 Oktoba 2025.

Wataalamu wa tasnia ya muziki kutoka duniani kote watakutana, kushirikiana, kujenga fursa mpya, na kubadilishana maarifa ya kina na mbinu za kiutendaji ili kuimarisha uchumi wa muziki kimataifa.

Tembelea Tovuti ya WOMEX 
Music in Africa ACCES Registration

ACCES 2025

Toleo la 8 la kongamano la ACCES linaloandaliwa na Music In Africa litafanyika katika jiji la Tshwane, Afrika Kusini, kuanzia tarehe 30 Oktoba hadi 1 Novemba 2025.

Tegemea burudani za kiwango cha juu, mijadala ya kitaaluma, fursa za kufanya mitandao ya kikazi kwa wataalamu wa muziki, na mengi zaidi.

Usajili umefunguliwa na unazingatia utaratibu wa kwanza kujisajili, kwanza kuhudumiwa.

Ni bure kabisa kwa washiriki kutoka Afrika!

Jisajili hapa  ACCES 2025!
Sauti za Busara Partners & Supporters
Sauti za Busara 2024 Audience

Mauzo ya  tiketi hugharamia asilimia 30 tu ya mahitaji ya tamasha la Sauti za Busara, na ingawa uendeshaji wa shughuli kuu unasaidiwa na Fumba Town kupitia CPS, bado tunawategemea wadau kama wewe kuhakikisha tamasha hili linaendelea kuishi na kustawi.

Kwa kuunga mkono Sauti za Busara 2026, unawekeza katika muziki wa Afrika, urithi wa kitamaduni, uwezeshaji wa vijana, na ukuaji wa sekta ya ubunifu barani Afrika.

Hii ni nafasi ya kipekee kulinganisha chapa yako na moja ya matamasha yanayoheshimika zaidi barani, na kuwasiliana moja kwa moja na hadhira ya kimataifa na yenye utofauti mkubwa.

Jiunge nasi kuifanya Sauti za Busara 2026 kuwa ya kukumbukwa — kwa wasanii, kwa jamii, na kwa mustakabali wa muziki wa Afrika.

Bofya hapa Kwa Udhamini!
Fumba Town Logo
Zanlink Logo (without LT) CMYK copy-1.png
Sauti za Busara - One Africa

Follow us on Social Media to get the latest updates:

This e-mail has been sent to [[EMAIL_TO]], click here to unsubscribe.

Busara Promotions. Maisara, Stone Town 3635 Zanzibar City TZ